Home » » BENKI YA CRDB YATWAA TUZO YA MWAJIRI BORA 2013

BENKI YA CRDB YATWAA TUZO YA MWAJIRI BORA 2013

Written By JAK on Tuesday, December 10, 2013 | 11:38 PM


Naibu Mkurugenzi Mtendaji-Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka akizungumza katika hafla ya utoaji Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka, ambapo benki hiyo ilikuwa moja ya wadhamini katika hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
 Makamu wa Rais Dk. Mohammed Gharib Bilal (kulia) akimkabidhi cheti Naibu Mkurugenzi Mtendaji-Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka kutokana na mchango wa benki hiyo katika kufanikisha sherehe za utoaji wa Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka (EYA 2013), ambapo benki hiyo ilikuwa moja ya wadhamini katika hafla hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki.
 Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka (kushoto) akimkabidhi, Naibu Mkurugenzi Mtendaji-Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka Tuzo ya Fedha ya ushindi wa pili ya Mwajiri Bora wa Mwaka (EYA 2013), zilizoandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE). Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa benki hiyo, Timoth Fasha. Sherehe hizo zilifanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. Benki ya CRDB, ilikuwa pia Mdhamini wa Fedha (Gold Sponsor) wa hafla ya kukabidhi tuzo kwa waajiri bora, ambapo ilikabidhiwa cheti cha udhamini.
Wadhamini wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal
Mkurugenzi wa tawi la Vijana, Pelesi Fungo.
Kaimu Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Willy Kamwela akipeana mkono na Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal.

Naibu Mkurugenzi Mtendaji-Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka akipeana mkono na Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal.
Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal (kushoto), akipeana mkono na Kaimu Mkurugenzi wa Rasirimali Watu wa Benki ya CRDB, Timoth Fasha.
Mkurugenzi wa tawi la Lumumba, John Almasi (kulia), Mkurugenzi wa tawi la Kijitonyama, Lucas Busigaz, Mkurugenzi wa tawi la Vijana, Peres Fungo, na Mwanasheria wa Benki ya CRDB wa pili kushoto na Ofisa Uhusiano wa Benki ya CRDB, Tumain Kamuhanda. 
Naibu Mkurugenzi Mtendaji-Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka akizungumza na waandishi wa habari. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa benki hiyo, Timoth Fasha.

DAR ES SALAAM, Tanzania

BENKI ya CRDB imefanikiwa kutwaa Tuzo ya Mwajiri Bora wa Mwaka 2013  (EYA), iliyotolewa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) na kufanyika jijini Dar es Salaam, hivyo kuendelea kuwa kinara miongoni mwa waajiri wa taasisi za fedha.

Akizungumza baada ya kukabidhiwa tuzo hiyo, Naibu Mkurugenzi Mtendaji-Huduma Shirikishi, Esther Kitoka, alisema CRDB inajivunia kiwango chake katika kuwajali na kuwathamini wafanyakazi, hivyo kuwawezesha kutwaa tuzo hiyo mara pili mfululizo.

Aliongeza kuwa, ili kuhakikisha wanafanikiwa kutwaa Tuzo ya Mwajiri Bora (EYA), ambayo mwaka huu imechukuliwa na Kampuni ya Simu ya Vodacom, wamejipanga kuboresha maafunzo miongoni mwa waajiriwa wao ili kuwaongezea ufanisi kazini.

“Mwakani tutakuwa na mafunzo ya wafanyakazi wetu katika Chuo Kikuu cha Milpark cha Afrika Kusini, ili kuboresha ufanisi miongoni mwa wafanyakazi na kurutubisha CV zao, vyote vikiwa ni kwa ustawi wa Benki CRDB na wateja wetu kwa ujumla,” alisema Kitoka.

Kitoka akasisitiza kuwa, kupitia mikakati hiyo, wanaamini mwakani Benki ya CRDB wataibuka washindi wa jumla (overall), hasa baada ya kutanua huduma zake hadi nje ya nchi kupitia matawi yake nchini Burundi na huduma za China UnionPay na China Desk.

Kwa upande wake Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka aliwapongeza washindi wote waliotwaa tuzo katika hafla hiyo, huku akiwataka kuboresha mazingira ya kazi miongoni mwa waajiriwa, kama ishara ya kuthamini mchango wao kwa kampuni na taifa.

Kabaka aliongeza kuwa, mhimili mkuu wa ukuaji wa uchumi wa nchi yoyote duniani ni utendaji uliotukuka miongoni mwa waajiriwa wa sekta rasmi na isiyo rasmi, ambao wasipoboreshewa mazingira, hawatokuwa wazalishaji wazuri kwa ustawi wa taifa.

Awali akifungua hafla hiyo, mgeni rasmi, Makamu wa Rais Dk Mohammed Gharib Bilal, aliwataka waajiri wote nchini kutumia hafla ya tuzo za Mwajiri Bora kama nia ya kujibu maswali lukuki kuhusu uzalishaji wa bidhaa na utawala bora mahali pa kazi.

Jumla ya tuzo 21 zilitolewa kwa kampuni mbalimbali zilizoshiriki katika mchakato huo uliokuwa chini ya udhamini mkuu wa Ultimate Security (Platinum Sponsor) na benki ya CRDB (Gold Sponsor) na kuratibiwa na ATE.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger