Pichani kati ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akifafanua jambo mbele ya wananfunzi
hao (hawapo pichani) baada ya kueleza kero zao. wengine kulia ni
Mwenyekiti wa CCM mkoa wa NJombe na Mbunge wa Njombe Kaskazini,Mh.Deo
Sanga kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Naoe Nnauye na katibu
wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Mbunge Mteule, Dk. Asha-Rose
Migiro.
Ndugu
Kinana na Ujumbe wake leo amekutana na Wanafunzi mbalimbali wa vyuo vya
elimu ya juu mkoani humo na kusikiliza changamoto na kero zao
mbalimbali na namna ya kuzifanyia kazi ikiwemo na kuzitatua.Kinana
amefanya ziara maalum ya kikazi katika mkoa huo wa Njombe,baada ya
kumaliza ziara yake ndefu ya mkoa wa Ruvuma na Mbeya,akiwa ameambatana
na Wajumbe wa kamati kuu ya CCM,Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya
Kimataifa,Dkt Asha-Rose Migiro pamoja na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi
Nape Nnauye.
Kama
vile haitoshi leo jioni kabla ya kurejea jijini Dar kwa njia ya Treni
ya TAZAR kutokea Makambako, Ndugu Kinana alishiriki uzinduzi wa albamu
ya kikundi cha Sanaa za Vichekesho cha mjini Njombe.
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na Wanafunzi hao jioni ya leo
katika chuo cha Maendeleo ya Jamii,kuhusiana na changamoto mbalimbali
zinazowakumba,mkoani Njombe.
Mkuu
wa Wilaya ya Njombe,Mh,Sarah Dumba akitoa sehemu ya ufafanuzi kuhusiana
na changamoto mbalimbali zinazokwamisha maendeleo katika chuo cha
Uuguzi Kibena,Mkoani Njombe wakati wa kujibu maswali ya wanafunzi wa
chuo hicho kama waonekanavyo pichani.
Mmoja
wa Wanafunzi wa Chuo cha Iringa akielezea changamoto mbalimbali
zinazowakabiri mbele ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na ujumbe wake
aliokuwa ameambatana nao.
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akionesha Albamu ya Amani Tanzania
iliyorekodiwa na kikundi cha vichekesho Sanaa Group,mkoani humo leo
katika uzinduzi uliofanyika mkoani Njombe mbele ya mashabiki wa kikundi
hicho,hawapo pichani.
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizindua Albamu ya Amani Tanzania
iliyorekodiwa na kikundi cha vichekesho Sanaa Group cha mkoani humo leo
katika uzinduzi uliofanyika mkoani Njombe mbele ya mashabiki wa kikundi
hicho,hawapo pichani.Anaeshuhudia pichani (koti jeusi) ni Mwenyekiti wa
Mkoa wa Njombe na Mbunge wa Njombe Kaskazini,Mh.Deo Sanga.
Pichani
shoto ni Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt Asha-Rose
Migiro wakijadiliana jambo na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe,Mh.Deo
Sanga pamoja na Katibu MKuu wa CCM,Ndugu Kinana wakati wa uzinduzi wa
albamu ya Amani Tanzania,ambapo wote walishiriki hafla hiyo.
Baadhi
ya Wanachama wapya wa CCM,kutoka vyuo vya juu mjini Njombe wakila kiapo
huku wakiwa wamezinyanyua kadi zao juu mara baada ya kukabidhiwa na
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mapema leo jioni.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akishiriki kupiga ngoma katika uzinduzi huo wa albamu ya Amani Tanzania.
KUTOKA Michuzi Blog
KUTOKA Michuzi Blog
Post a Comment