Home » » KINANA AKUTANA NA WASOMI CCM VYUO VYA ELIMU YA JUU, NJOMBE LEO,ASHIRIKI UZINDUZI WA ALBAMU YA VIJANA

KINANA AKUTANA NA WASOMI CCM VYUO VYA ELIMU YA JUU, NJOMBE LEO,ASHIRIKI UZINDUZI WA ALBAMU YA VIJANA

Written By JAK on Sunday, December 8, 2013 | 3:38 AM



Pichani kati ni Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akifafanua jambo mbele ya wananfunzi hao (hawapo pichani) baada ya kueleza kero zao. wengine kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa NJombe na Mbunge wa Njombe Kaskazini,Mh.Deo Sanga kushoto ni Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Naoe Nnauye na katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Mbunge Mteule, Dk. Asha-Rose Migiro.

Ndugu Kinana na Ujumbe wake leo amekutana na Wanafunzi mbalimbali wa vyuo vya elimu ya juu mkoani humo na kusikiliza changamoto na kero zao mbalimbali na namna ya kuzifanyia kazi ikiwemo na kuzitatua.Kinana amefanya ziara maalum ya kikazi katika mkoa huo wa Njombe,baada ya kumaliza ziara yake ndefu ya mkoa wa Ruvuma na Mbeya,akiwa ameambatana na Wajumbe wa kamati kuu ya CCM,Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt Asha-Rose Migiro pamoja na Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.

Kama vile haitoshi leo jioni kabla ya kurejea jijini Dar kwa njia ya Treni ya TAZAR kutokea Makambako, Ndugu Kinana alishiriki uzinduzi wa albamu ya kikundi cha Sanaa za Vichekesho cha mjini Njombe.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizungumza na Wanafunzi hao jioni ya leo katika chuo cha Maendeleo ya Jamii,kuhusiana na changamoto mbalimbali zinazowakumba,mkoani Njombe.
Mkuu wa Wilaya ya Njombe,Mh,Sarah Dumba akitoa sehemu ya ufafanuzi kuhusiana na changamoto mbalimbali zinazokwamisha maendeleo katika chuo cha Uuguzi Kibena,Mkoani Njombe wakati wa kujibu maswali ya wanafunzi wa chuo hicho kama waonekanavyo pichani.
Mmoja wa Wanafunzi wa Chuo cha Iringa akielezea changamoto mbalimbali zinazowakabiri mbele ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na ujumbe wake aliokuwa ameambatana nao.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akionesha Albamu ya Amani Tanzania iliyorekodiwa na kikundi cha vichekesho Sanaa Group,mkoani humo leo katika uzinduzi uliofanyika mkoani Njombe mbele ya mashabiki wa  kikundi hicho,hawapo pichani.

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akizindua Albamu ya Amani Tanzania iliyorekodiwa na kikundi cha vichekesho Sanaa Group cha mkoani humo leo katika uzinduzi uliofanyika mkoani Njombe mbele ya mashabiki wa  kikundi hicho,hawapo pichani.Anaeshuhudia pichani (koti jeusi) ni Mwenyekiti wa Mkoa wa Njombe na Mbunge wa Njombe Kaskazini,Mh.Deo Sanga.
Pichani shoto ni Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt Asha-Rose Migiro wakijadiliana jambo na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe,Mh.Deo Sanga pamoja na Katibu MKuu wa CCM,Ndugu Kinana wakati wa uzinduzi wa albamu ya Amani Tanzania,ambapo wote walishiriki hafla hiyo.
Baadhi ya Wanachama wapya wa CCM,kutoka vyuo vya juu mjini Njombe wakila kiapo huku wakiwa wamezinyanyua kadi zao juu mara baada ya kukabidhiwa na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mapema leo jioni.
Katibu wa NEC,Itikadi na Uenezi,Nape Nnauye akishiriki kupiga ngoma katika uzinduzi huo wa albamu ya Amani Tanzania.

KUTOKA Michuzi Blog
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger