Home » , » Rais Kikwete akutana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa New York

Rais Kikwete akutana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa New York

Written By JAK on Thursday, December 26, 2013 | 3:03 AM


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,Ban Ki Moon akimkaribisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwaajili ya kufanya mazungumzo nae.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Ban Ki Moon akimkaribisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwenye ofisi yake iliyopo Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani jana
Bwana Ban Ki Moon na Rais Mrisho Kikwete wakijadili jambo ambapo masuala mbalimbali ya kimataifa hususan masuala ya amani na ushiriki wa majeshi ya Tanzania katika kudumisha amani sehemu mbalimbali Afrika na katika nchi nyingine duniani yalijadiliwa, ambapo Tanzania ikiwa ina majeshi ya kulinda amani katika nchi kadhaa ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Darfur nchini Sudan na Lebanon. Rais Kikwete yupo jijini  New York nchini Marekani ambapo anaendelea vyema na ukaguzi wa kawaida wa afya yake.
Bwana Ban Ki Moon na Rais Mrisho Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja
 (Picha na Freddy Maro)

Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger