Home » » WATOTO WALEMAVU WATEMBELEWA NA MAMA SALMA KIKWETE

WATOTO WALEMAVU WATEMBELEWA NA MAMA SALMA KIKWETE

Written By JAK on Monday, April 21, 2014 | 10:29 PM


MAMA SALMA KIKWETE ATEMBELEA KITUO CHA WALEMAVU CHA RASIBURA LINDI NA KUTOA ZAWADI YA PASAKA

 Baadaye Mama Salma anaonekana akipiga picha naye akiwa amelala kitandani kwani Theresia hawezi kukaa wala kusimama
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akikaribishwa kwenye kituo cha walemavu cha Rasibura na Ndugu Simon Mnimbo, Mkurugenzi wa Shirika la Caritas la Kanisa Katoliki Jimbo la Lindi wakati Mama Salma alipokitembelea kituo hicho tarehe 20.4.2014, siku ya Pasaka kwa ajili ya kuwapelekea zawadi  za sikukuu.
 Jengo linalotumika kwa makazi ya walemavu huko Rasibura, katika Mji wa Lindi likiwa katika hali mbaya ya uchakavu. Jengo hilo awali lilikuwa likitumiwa kama gereza na Jeshi la Magereza la Lindi na baadaye kukabidhiwa kwa Idara ya Ustawi wa Jamii na ndipo walipoamua kutumia kama jengo la kuwatunzia watu wenye ulemavu.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitembelea sehemu mbalimbali za jengo la kuwatunzia walemavu huko Rasibura Mjini Lindi akiongozwa na Mlezi wa Kituo hicho Ndugu Simon Mnimbo kutoka Kanisa Katoliki Jimbo la Lindi
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitembelea sehemu mbalimbali za jengo la kuwatunzia walemavu huko Rasibura Mjini Lindi akiongozwa na Mlezi wa Kituo hicho Ndugu Simon Mnimbo kutoka Kanisa Katoliki Jimbo la Lindi
 Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akiongea na watu wenye ulemavu mbalimbali wanaoishi Rasibura baada ya kutembelea sehemu mbalimali za jengo lao. Mama Salma aliwatembelea walemavu hao wakati wa sikukuu ya pasaka na kuwapa zawadi mbalimbali za sikukuu hiyo
  Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na mtoto Idd Mohamed Chitawala ambaye ni mlemavu wa macho anayeishi katika kituo cha rasibura pamoja na Baba yake Mzazi Bwana Mohamed Chitawala.
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkabidhi Kiongozi wa Kituo cha walemavu cha Raisbura Bwana Mohamed Chitawala baadhi ya vyakula alivyowaletea- mchele, unga, mafuta ya kupikia, sukai, soda na vinginevyo wakati alipotembelea kituo cha walemavu cha Rasibura huko Lindi siku ya Pasaka
 Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimkabidhi zawadi yake ya Pasaka Ndugu Theresia Thomas ambaye ni mlemavu wa viungo anayeishi katika kituo cha Rasibura huko Lindi. Baadaye Mama Salma anaonekana akipiga picha naye akiwa amelala kitandani kwani Theresia hawezi kukaa wala kusimama.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na baadhi ya watu wenye ulemavu wanaoishi katika Kituo cha Rasibura mara baada ya kuwakabidhi zawadi zao za Pasaka. Picha na John Lukuwi
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger