Home » » Moto wazuka katika stoo ya chuo cha taaluma ya Polisi Moshi

Moto wazuka katika stoo ya chuo cha taaluma ya Polisi Moshi

Written By JAK on Thursday, February 13, 2014 | 12:07 AM

Wanafunzi wa chuo cha taaluma ya polisi Moshi wakijaribu kuzima moto na kuokoa mali zilizokuwa zikiungua katika moja ya stoo ya kuhifadhia vitu mbalimbali zikiwemo nguo baada ya kuzuka kwa moto katika jengo hilo. Hakuna mtu aliyeripotiwa kudhurika na Mkuu wa Chuo hicho Kamishana Msaidizi wa Polisi Matanga Mbushi ameahidi kutoa taarifa kamili baadaye. 
Askari wanafunzi wakipambana na moto kwa kila jinsi
Mapambano na moto yanaendelea
Baadhi ya vitu vikiokolewa kutoka katika jengo lililowaka moto.
Juhudi za kuondoa vifaa vilivyookolewa kabla ya kuteketea kwa moto
Wanafunzi wakipambana na moto





Sare za askari zikiwa zimeokolewa toka katika jengo hilo.
Moja ya kifaa kilichopo chuoni hapo ambacho pia kilikuwa kikitumika kwa shughuli za kuzima moto katika jengo hilo .Mkuu wa chuo hicho Matanga Mbushi amesema taarifa kamili ya moto huo itatolewa baadae.

Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Robert Boaz akiwa na mkuu wa Chuo cha taaluma ya Polisi kamishana msaidizi wa polisi Matanga Mbushi wakishuhudia zoezi la uzimaji moto katika jengo hilo.





Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger