Home » » Watu wawili wahukumiwa faini shilingi milioni 15 ama jela miaka 15 kwa ujenzi wa jengo la ghorofa 18 jijini Dar es Salaam

Watu wawili wahukumiwa faini shilingi milioni 15 ama jela miaka 15 kwa ujenzi wa jengo la ghorofa 18 jijini Dar es Salaam

Written By JAK on Monday, February 10, 2014 | 9:50 PM

Watu  wawili wamehukumiwa kulipa faini ya Sh. Milioni 15 au kwenda jela miaka miaka 15 baada ya kupatikana na hatia ya makosa matano ya ujenzi wa jengo la ghorofa 18 lililojengwa jirani na Ikulu lililopo mtaa wa Chimala Kitalu cha 45 na 46, kinyume cha sheria. 
 Washtakiwa hao ni aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Makumba Kimweri na aliyekuwa Msanifu Mkuu wake Richard Maliyaga (55) wote wakazi wa jijini Dar es Salaam. 
 Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Sundi Fimbo alisema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na upande wa mashitaka dhidi ya washtakiwa, mahakama imeona wana hatia kwa makosa yote matano. 
 Alisema hati ya mashitaka inaonyesha mshtakiwa wa kwanza anakabiliwa na mashitaka watatu na upande wa mashitaka umethibitisha kweli alitenda makosa hayo na mahakama inamhukumu kulipa faini ya Sh. Milioni 3 kwa kila kosa au kulipa faini ya Sh. Milioni 3 kwa kila kosa. 
 Kwa upande wa mshtakiwa wa pili, hakimu alisema hakuna ubishi bila kuacha shaka mshtakiwa, alitenda makosa hayo na kwamba atalipa faini ya Sh. Milioni 3 kila kosa au kulipa fani ya Sh. Milioni 3 kila kosa. Hata hivyo, walilipa faini hiyo na kuachiwa huru.
 Katika kesi ya msingi, washtakiwa walikuwa wakikabiliwa na mashitaka matano ya matumizi mabaya ya ofisi katika utoaji kibali cha ujenzi wa jengo la ghorofa 15 kiwanja namba 45 mtaa wa Chimara.
 Ilidaiwa kuwa Kimweri alikuwa na wadhifa huo TBA kuanzia mwaka 2002 hadi 2010 na Maliyaga aliajiriwa mwaka 2002 akiwa msanifu mkuu.
 Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Leonard Swai alidai kiwanja hicho kilikuwa kinamilikiwa na TBA, ambako hadi mwaka 2006 kilikuwa hakijaendelezwa. 
 Aidha TBA, kwa mujibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma iliwaalika wanaotaka kuwekeza kuwasilisha andiko la awali kwa ajili ya uendelezaji.
Wote wamelipa faini na kuachiwa huru
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger