Home » » RAIS KIKWETE APOKEA UJUMBE MAALUM TOKA KWA RAIS ZUMA WA AFRIKA KUSINI IKULU, DAR ES SALAAM

RAIS KIKWETE APOKEA UJUMBE MAALUM TOKA KWA RAIS ZUMA WA AFRIKA KUSINI IKULU, DAR ES SALAAM

Written By JAK on Monday, March 17, 2014 | 11:36 AM


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono  na Mjumbe Maalum wa Rais wa Afrika Kusini Mhe. Maite Nkoana-Mashabane, ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Ikulu jijini Dar es salaam leo.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Mjumbe Maalum wa Rais wa Afrika Kusini Mhe. Maite Nkoana-Mashabane, ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa nvhi hiyo Ikulu jijini Dar es salaam leo.
Picha na Ikulu


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo,

Jumapili, Machi 16, 2014, amepokea ujumbe maalum kutoka kwa Rais Jacob Zuma wa

Afrika Kusini.


Ujumbe huo wa Rais Zuma umewasilishwa kwa Rais Kikwete na Waziri wa Mambo ya Nje wa

Afrika Kusini, Mheshimiwa Maite Nkoana-Mashabane wakati mama huyo alipokutana

na kufanya mazungumzo na Rais Kikwete, Ikulu, Dar Es Salaam.


Mara baada ya kuwasilisha ujumbe huo, viongozi hao wamejadili masuala yanayohusu

uhusiano kati ya Tanzania na Afrika Kusini na masuala ya kikanda ambako nchi

zote mbili ni wanachama wa Jumuia ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).


Mheshimiwa Nkoana-Mashabane ameondoka nchini mara baada ya kuwasilisha ujumbe 

huo kwa Rais Kikwete. 


Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
16 Machi,2013



Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger