Home »
Sport
» MTANZANIA KUWANIA UBINGWA WA DUNIA WA WBC KWA MARA YA KWANZA
MTANZANIA KUWANIA UBINGWA WA DUNIA WA WBC KWA MARA YA KWANZA
Omari Kimweri
BONDIA MTANZANIA Omari
Kimweri 'Lion Boy' anaefanya shughuli zake Deer Park, Victoria,
nchini
Australia anatarajia kuwa mtanzania wa kwanza kupanda ulingoni kugombea ubingwa
wa Dunia unaotambuliwa na WBC uzito wa
kg47.5minimum weight.
Mpambano huo utakaopigwa nchini China November 30, 2013 Mchina Xiong Zhao Zhong
ambaye ni bingwa wa
dunia wa WBC ambaye anashikilia taji hilo kwa sasa katika uzito huo
Kimweri anakuwa mtanzania wa kwanza kuwania taji kubwa
kabisa Duniani akitokea nchini Austalia.
Omari Kimweri na Randy petalcoria
Kigezo cha kufanya apate pambano hilo kubwa ni kutokana na
rekodi yake pamoja na kutakiwa mtu ambaye anatokea bara la Afrika ambapo kura
imemdondokea bondia Omari Kimweri, ambapo ni kiu ya mabondia wengi duniani
kumiliki mikanda mikubwa ya kimataifa. Kimweri mwenye rekodi ya kucheza michezo 16 ambapo ameshinda
michezo 13 na kuchezea kichapo michezo 3
wakati mpinzani wake Xiong Zhao
Zhong amecheza michezo 26 akishinda 21 kupigwa 4 na kutoka droo moja.
Mabondia hao wote wana umri wa miaka 31, wakitofautiana kwa mwezi mmoja tu
katika kuzaliwa. Mpambano wao umekuwa gumzo katika dunia ambapo kila mmoja
anajiandaa kwa nguvu
Kimweri kwa sasa anaefanya mazoezi makali, akipewa sparring
na bondia Randy Petalcoria wa
Philippines ambaye ni bingwa wa light fly weight.
Omari Kimweri kwa sasa yupo katika mazoezi mazito ya
kujiandaa na mpambano huo, akitegemea
zaidi dua za Watanzania kwa kuwa ushindi
wake ni ushindi wa watanzania wote.
Mungu Ibariki
Tanzania
Mungu Mbariki Bondia Omari Kimweri
Post a Comment