Mshitakiwa, Sharif Mohamed Athuman (31), ambaye ni
mshitakiwa namba moja katika kesi ya Mauaji ya Bilionea wa Madini ya Tanzanite,
Erasto Msuya mchimbaji mdogo wa madini na mkazi wa Kimandolu mkoani Arusha, akitoka
nje ya Mahakama ya Hakimu mkazi Moshi, muda mfupi baada ya kesi hiyo
kuahirishwa hadi Desemba 11, mwaka huu.
Mshitakiwa namba mbili, Shaibu Jumanne Saidi maarufu kama
Mredi (38),anayetuhumiwa na wengine saba, kumuua Mfanyabiashara Erasto Msuya
kwa kumpiga risasi akitoka kwa taabu nje ya mahakama ya Hakimu mkazi Moshi,
baada ya kesi hiyo kuahirishwa hadi Desemba 11, mwaka huu.
Mmoja wa Washtakiwa katika kesi ya Mauaji, anayetuhumiwa
kushirikiana na wenzake saba, kumuua Mfanyabiashara Erasto Msuya kwa kumpiga
risasi akisindikizwa na Maaskari kutoka katika mahakama ya Hakimu mkazi Moshi,
muda mfupi baada ya kesi hiyo jana kuahirishwa hadi Desemba 11,mwaka huu.
Washitakiwa Joseph Damian "Chusa" na mwenzake
Shaibu Jumanne Saidi "Mredi", wakimsaidia Mshitakiwa mwenzao kupanda
katika Gari la Polisi muda mfupi baada ya kesi inayowakabili ya mauaji ya
Bilionea wa Madini ya Tanzanite, Erasto Msuya kuahirishwa hadi Desemba 11,
mwaka huu.
Post a Comment