WA MAPITIO YA
UTENDAJI WA SEKTA YA UCHUKUZI (JTSR 2013) UNAOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO
WA JENGO LA GOLDEN JUBILEE (PSPF BUILDING) ,JIJINI DAR ES SALAAM TAREHE 28-29
OKTOBA 2013
Waziri wa Uchukuzi,
Dkt. Harrison Mwakyembe akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 7
wa mapitio ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi leo asubuhi katika ukumbi wa
mikutano uliopo kwenye Jengo la Golden Jubilee(PSPF BUILIDNG). Mkutano huo wa
siku mbili unakutanisha wadau wa taasisi mbalimbali za sekta ya uchukuzi
kujadili njia mbalimbali za kuboresha sekta ya Uchukuzi.
Washiriki wa mkutano
wa 7 wa Mapitio ya Utendaji wa sekta ya Uchukuzi, wakijitambulisha kabla ya
mkutano huo wa siku mbili kuanza katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Jubilee.
Mkutano huo wa 7 unawakutanisha wadau
mbalimbali wa sekta ya Uchukuzi kujadili changamoto mbalimbali zinazoikabili
sekta na kuzitafutia ufumbuzi.
Katibu Mkuu wa Wizara
ya Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa Mkutano
7 wa mapitio ya utendaji wa Sekta ya Uchukuzi(JTSR 2013), unaofanyika katika
ukumbi wa mikutano Jengo la Golden Jubilee tarehe 28-29 Oktoba 2013. Mkutano
huo wa 7 unawakutanisha wadau
mbambali wa sekta ya uchukuzi kujadili changamoto mbalimbali
zinazoikabili sekta ya uchukuzi na kuzitafutia ufumbuzi ili kuboresha Uchukuzi
nchini Tanzania. ![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhDWlZnIbMUF_3ObOKVyKaVuMveSzh4fF-9bklEsOlAzlD-BpFng4usdi1plr-aRPt87qI4l4TRK7Qvs54ZiYnJB-IUzT3gFEFGDgOMpbDaNFmiuzMU7GCzAFc3_OXqNAKMF_2dBExmf8ak/s640/DSC_0029.JPG)
Katibu Mkuu wa Wizara
ya Ujenzi Mhandisi Alhaj Mussa Iyombe, akitoa hotuba yake wakati wa ufunguzi wa
mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa Sekta ya Uchukuzi leo asubuhi katika
ukumbi wa mikutano katika Jengo la Golden Jubilee.
Waziri wa Uchukuzi,
Dkt. Harrison Mwakyembe (wa tatu kutoka kushoto waliokaa), akiwa katika picha
ya pamoja na Mabalozi, wahisani wa Miradi ya Maendeleo na wajumbe mbalimbali
waliohudhuria mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa sekta ya Uchukuzi,
Unaofanyika tarehe 28-29 Oktoba katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la Golden
Jubilee. Wa kwanza kushoto waliokaa ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi,
Mrs. Monica Mwamunyange, kulia kwa Waziri Mwakyembe ni Katibu Mkuu wa Wizara ya
Uchukuzi, Dkt. Shaaban Mwinjaka.
Mkurugenzi Msaidizi wa Sehemu ya Usimamizi, Ufuatiliaji na
Tathimini wa Wizara ya Uchukuzi , Bw. Aunyisa Meena, akiwasilisha mada kwenye
mkutano wa 7 wa mapitio ya utendaji wa sekta ya
Uchukuzi, unaofanyika Tarehe 28-29 Oktoba katika ukumbi wa
mikutano wa Jengo la Golden Jubilee. Mkutano huo utajadili maswala mbalimbali
yanayohusu sekta ya Uchukuzi.
Habari na picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)
Post a Comment