Home » » Naibu wa mkuu wa usalama atekwa Libya

Naibu wa mkuu wa usalama atekwa Libya

Written By JAK on Monday, November 18, 2013 | 6:58 AM


Wanamgambo wa Libya
Naibu wa mkuu wa usalama wa Libya, Moustapha Nouh, ametekwa nyara kutoka uwanja wa ndege wa Tripoli alipokuwa akirudi nchini.
Kamanda mmoja piya alitekwa lakini aliweza kukimbia na alieleza kuwa walitekwa na watu wasiojulikana waliokuwa na silaha.
Afisa huyo ametekwa wakati kunafanywa mgomo katika mji mkuu kuwahimiza wapiganaji waondoke katika mji huo.

Mgomo umefanywa baada ya zaidi ya watu 40 kufa na mamia kujeruhiwa kwenye mapambano ya siku mbili baina ya wanamgambo na waandamanaji, ambao wamewaomba wanamgambo waondoke mjini.
Waziri Mkuu, Ali Zeidan, alitekwa nyara kwa muda mfupi mwezi uliopita.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger