Home » » NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE ATUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE ATUNUKIWA SHAHADA YA UZAMIVU

Written By JAK on Monday, November 18, 2013 | 6:21 AM


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akitafakari wakati wa Mahafali ya 43 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo Mhe. Dkt. Maalim alitunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika masuala ya Sheria.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Mhe. Balozi Fulgence Kazaura akimtunuku Shahada ya Uzamivu (Ph.D) Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) katika Mahafali ya 43 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani tarehe 16 Novemba, 2013. Mhe. Dkt. Maalim alikuwa miongoni mwa Wahitimu 41 waliotunukiwa Shahada ya Uzamivu siku hiyo.
Mhe. Dkt. Maalim na Wahitimu wengine wa Shahada ya Uzamivu wakiwa wenye nyuso za furaha.
/td>
Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam, Mhe. Balozi Fulgence Kazaura (katikati mwenye joho jekundu) akiwa na Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Prof. Rwekaza Mukandala (wa tatu kutoka kushoto) pamoja na Wahadhiri wengine wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakati wa Mahafali ya 43 ya Chuo hicho.
Wahitimu wa Shahada na Stashahada mbalimbali.
Picha ya pamoja
Mhe. Dkt. Maalim (katikati) akiwa na Wahitimu wenzake. Kushoto ni Dkt. Adelardus Kilangi na Dkt. Mramba Joseph (kulia)
Mhe. Dkt. Maalim akiwa na Wahitimu wengine wakiimba Wimbo wa Taifa.
Mhe. Dkt. Maalim akiwa na Mke wake mara baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamivu.
Share this article :

Post a Comment

Mhe. Dkt. Maalim na Familia yake.

My Blog List

Trending Topic

Sample Text

Followers

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger