Home » » BAADA YA KIPIGO CHA 3-1 NA SIMBA JUZI KATIKA 'BONANZA' YA NANI MTANI JEMBE, YANGA YAMTIMUA KOCHA WAKE ERNIE BRANDTS

BAADA YA KIPIGO CHA 3-1 NA SIMBA JUZI KATIKA 'BONANZA' YA NANI MTANI JEMBE, YANGA YAMTIMUA KOCHA WAKE ERNIE BRANDTS

Written By JAK on Tuesday, December 24, 2013 | 1:56 AM


Masaa 24 tu baada ya  Yanga kupigwa mabao 3-1 dhidi ya wapinzani wao Simba, uongozi wa klabu hiyo umemfungashia virago kocha wake Ernie Brandts, kufuatia uamuzi wa kikao cha kamati ya utendaji ya Yanga iliyoketi muda mchache baada ya mchezo wao na Simba. 

Mwenyekiti wa kamati ya usajili Abdallah Binklebu amesema leo jijini Dar es salaam kuwa wamefikia uamuzi huo baada ya kupokea maoni ya wachezaji mbali mbali wa zamani kuhusu kiwango cha timu. 

 "Tumempa notisi ya siku 30 ili tuendelee kutafuta kocha mwingine, na tupo kwenye mchakato wa kumlipa stahiki zake, tuachane kwa amani. 
 “Mwanzoni alipandisha kiwango cha timu, kilipanda sana, lakini baadaye kiwango kikaanza kushuka, tukasema tumpe muda kidogo, lakini tunaona mambo yanazidi kuharibika, hivyo tumeamua kuachana naye kwa sababu hana jipya, sisi tunalenga michuano ya kimataifa zaidi sasa kwa kiwango hichi hatutafika mbali ni lazima tuchukue hatua za haraka zaidi,”alisema. 

 Kuhusu Wajumbe wengine wa benchi la Ufundi, Bin Kleb alisema kwamba taratibu nyingine zinafuata na ndani ya wiki hii kuna maamuzi mengi makubwa ambayo klabu yake itayafanya. 
 Hata hivyo tayari Brandts alikabidhiwa barua yake ya kusitishiwa mkataba rasmi juzi na jana baada ya mazoezi Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Clement Sanga alikutana na wachezaji na kuzungumza nao kwa zaidi ya nusu saa. 
Kocha Brandts amesema  kwa kifupi "Nasubiri notisi ya siku 30 imalizike. Kuna kitu nitaongea lakini sio sasa. Sasa hivi msikilizeni Abdallah (Binkleb) anachosema ukifika muda na mimi nitazungumza."
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger