katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na ujumbe wake wakizungumza
na Wafanyakazi wa TAZARA-Iyunga,Wilayani Mbeya mjini Mkoani Mbeya
mapema leo,kuhusiana na matatizo mbalimbali yanayoikabiri shirika hilo
nchini.
Kinana
alisikiliza changamoto mbalimbali kutoka kwa Uongozi wa Shirikia hilo
ikiwemo suala la Uchakavu wa mitambo na vitendea kazi,Upatikanaji wa
Mafuta ya kuendeshea mitambo,Upungufu wa wafanyakazi,Kutolipwa
Mishaharaya Wafanyakazi kwa wakati,Makato ya malimbikizo Michango ya
Wafanyakazi kupeleka NSSF,Mafao kuchukua mda mrefu,Hujuma mbalimbali
ndani ya shirika hilo, ukosefu wa magari na changamoto nyinginezo.
Ndugu
Kinana katika kujibu na kutoa ufafanuzi wa changamoto hizo,alizipokea
na kuomba kuzifanyika kazi ipasavyo na kuhakikisha TAZARA
inaimarika.Aidha aliongeza kwa kusema kuwa kuna baadhi ya Changamoto
zinatokana na baadhi ya wenye Malori kufanya hujuma mbalimbali
kuhakikisha TAZARA inaendelea kudidimika kila kukicha,kwamba hawapendi
TAZARA ifufuke,Kwa hivyo tutafute namna ya kuimarisha TAZARA
Wafanyakazi
wa Shirika la TAZARA wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana
alipozungumza nao mapema leo,kwenye ukumbi wa mikutano wa shirika hilo
mara alipowasili na ujumbe wake kutokea Mbeya Vijijini katika ziara ya
kukiimarisha chama cha CCM.
Mmoja
wa wafanyakazi wa TAZARA,aliyejitambulisha kwa jina la Maulid Said
akzizungumza kuhusiana na hujuma mbalimbali zinazofanywa na baadhi ya
watu ya kuhakikisha shirika hilo haliendelei,aidha ameitupia lawama
Serikali kwa kuacha barabara zetu zikiharibika kila kukicha na Malori ya
Mizigo kwa kuzidisha uzito huku ikishindwa kuliimarisha shirika la TAZARA ambalo lingeweza kupunguza ama kuliondoa kabisa tatizo hilo.
Mfanyakazi
wa TAZARA,aliyejitambulisha kwa jina la Seif Rashid akiuliza swali
kuhusu suala la Mafao katika shirika hilo la TAZARA,akibainisha kuwa
limekuwa tatizo sugu kwa Wafanyakazi wastaafu.
Mmwenyekiti
wa Kamati ya Uongozi wilaya (Mbeya) TAZARA,Ali Mkami akisoma hotuba fupi mbele ya
Katibu Mkuu wa CCM na Ujumbe wake uliofika kwenye shirika hilo na
kuzisikiliza kero na changamoto mbalimbali zilizopo.
Mbunge
wa Viti Maalum Mkoani Mbeya Mary Mwanjelwa akiwasalimia Wafanyakazi wa
TAZARA waliofika kuzungumza na Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Ujumbe
wake,akiwemo Katika wa NEC,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye,Katibu wa
NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt.Asharose Migiro.Ndugu Kinana na
Ujumbe wake leo wako Mbeya mjini kuhitimiza ziara yao ya Kuimarisha
chama cha CCM,Ziara hiyo ilianzia Mkoa wa Ruvuma na Mbeya na Njombe.
Wafanyakazi wa TAZARA wakisikiliza kwa makini
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na uongozi wa TAZARA,Pichani kati Mkuu wa Wilaya ya Mbeya ,Mh.Norman Sigalla na shoto ni Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt.Asharose Migiro.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Ujumbe wake,Katika wa NEC,Itikadi na Uenezi Nape Nnauye,Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt.Asharose Migiro walipokuwa wakiwasili katika kijiji cha Iwambi kata ya Iwambi,Wilaya Mbeya mjini,mkoani Mbeya katika ziara ya Kukiimarisha chama chao.
Vijana na mambo yao wakimkaribisha Ndugu Kinana na ujumbe wake.
WAFANYAKAZI WA TAZARA WAOMBA TAZARA ICHUKULIWE NA WACHINA..!
Post a Comment