Mbunge wa jimbo la Iringa mjini kupitia chama cha CHADEMA,Mch. PETER MSIGWA, amekanusha kuhusiana na tuhuma zinazomkabili juu
ya kutokabidhi fedha za rambirambi kiasi cha shilingi milioni moja kwa mjane wa
aliyekuwa mwenyekiti wa chama cha wandishi wa habari mkoa wa Iringa marehemu DAUDI
MWANGOSI, ambazo zilitolewa na wanachama wa CHADEMA waliopo nchini Uingereza na
kusema kuwa tuhuma hizo si za ukweli, ni mambo ya uzushi na kwamba watu wanasema
hivyo ili kumchafua .
Akizungumza na na kituo cha redio ya Nuru fm ya Iringa,kupitia kipindi cha sunrise power,Mh. MSIGWA amesema kuwa ni kweli pesa hizo
alipokea kupitia kwa MAJID MGENGWA na baada ya kupokea fedha hizo alichangisha
tena fedha kwa wananchi wa jimbo la Iringa mjini kupitia mkutano, ambapo walichangia
kiasi cha laki tatu pamoja na yeye mwenyewe aliongezea kiasi cha shiringi
laki tano ,hivyo kupelekea kufikia kiasi cha shiringi milioni moja na laki nane
na sitini na nane na kumkabidhi mjane wa marehemu DAUDI MWANGOSI.
Msigwa amesema kuwa ni
wanasiasa tu wanaojaribu kuwachafua baada ya kuona kuwa wameshindwa na tayari
amewasiliana na uongozi wa chama chake ili kuweza kulichukulia hatua gazeti
ambalo limeandika tuhuma hiyo.
Post a Comment