Home » » Msajili wa Vyama Vya Siasa awataka wana Arusha kuacha ushabiki wa kisiasa unaohatarisha Amani...!!

Msajili wa Vyama Vya Siasa awataka wana Arusha kuacha ushabiki wa kisiasa unaohatarisha Amani...!!

Written By JAK on Sunday, December 8, 2013 | 5:21 AM

LEMA AKIMBIA MKUTANO WA KUITAKIA AMANI MKOA WA ARUSHA


Wadau wa amani wakiwa jukwaa kuu wakiwa wanafuatilia matukio mbali mbali ya maadhimisho ya kuutakia amani mkoa wa Arusha baada ya kukumbwa na matukio mbali mbali yaliotokea baada ya uchaguzi mkuu na mabomu kwenye kanisa la Joseph mfanyakazi olasit na Soweto mkutano ulioandaliwa na msajili wa vyama vya siasa na vyama vya siasa mkoani hapa na kufanyika  kwenye uwanja wa kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini hapa.
 Mmoja wa washiriki akiwaonyesha viongozi na wananchi wa jiji la Arusha hawapo pichani waliohudhuria hafla hiyo bango lisemalo amani kwanza vyama baadae ujumbe ulioendana na siku hiyo mbele ya msajili wa vyama vya siasa jaji Francis Mutungi na mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo na viongozi wa vyama vya siasa na dini mkoani hapa.
 Sehemu ya umati mkubwa wa wananchi na wakazi wa mkoa wa Arusha walioshiriki kuiombea amani mkoa wa Arusha wakifuatilia matukio mbali mbali yaliokuwa yakiendelea uwanjani
 Mchungaji Christopher Mwakasege akiombea amani ya mkoa wa Arusha kwenye siku hiyo ya kusahau tofauti na matukio yaliotokea kwenye mkoa huu wakati na baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 kwenye uwanja wa sheikh Amri Kaluta Abeid
 Juu na chini wanaonekana viongozi mbali mbali wa serikali, vyama vya siasa na dini mkoani Arusha Pamoja na mgeni Rasmi Jaji Francis Mutungi Msajili wa Vyama vya siasa wakiwa kwenye maombi yaliokuwa yakiombwa na mwalimu na mchungaji Christopher Mwakasege kwenye uwanja wa sheikh Amri Kaluta Abeid.



Baadhi ya bendera za vyama vya Kisiasa na serekali zikipepea uwanjani hapo.



Umati wa Wana Arusha waliohudhuria katika mkutano huo kwa ajili kuitakia mema mkoa wa Arusha


Baadhi ya Wanahabari wakifuatilia kwa karibu.
Sehemu ya umati wa watu wakifuatilia matukio kwa karibu.
Wanahabari wakiwa mzigoni.
Jaji Francis Mutungi Msajili wa Vyama vya siasa akiteta jambo na Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Wilaya ya Arusha Ndg Jasper Kishumbua akimpongeza mgeni rasmi kwa kazi nzuri aliyoianzisha,mara baada ya Mkutano huo.
Wadau mbalimbali akiwemo Katibu wa Uchumi na Fedha wa CCM Wilaya ya Arusha Ndg Victor Mollel (katikati aliyevaa sweta)


Msajili  wa vyama vya siasa  nchini  Jaji Fransis  Mutungi  amewataka  wananchi  wa  Mkoa  wa  Arusha na Watanzania  kwa  ujumla   kuepuka kuingiza  ushabiki  kwenye  siasa  kwani   kufanya  hivyo  licha ya kuwa  chanzo   cha kuhatarisha  amani  wanaharibu   lengo  la  fani hiyo  ambayo ina  umuhimu  na  faida  kubwa  katika  jamii   kama  taratibu  na misingi yake  ikifuatwa   na kuheshimiwa .

Akizungumza  na wananchi na viongozi wa  ngazi mbalimbali  za  Mkoa  wa  Arusha  waliokusanyika  katika  uwanja  wa  Shekh Amri  Abeid  kuuombea mkoa  wa Arusha amani  Jaji Mutungi  amesema amani ndio msingi  wa  kila  kitu  na  haihusiani kabisa  na  siasa hivyo  hakuna sababu ya  watanzania  kukubali  amani  iliyopo isivurugwe  na  watu  wachache  wanaosingizia  siasa  kwani  wanaopenda amani  ni  wengi  kuliko  wanasiasa.


Wakizungumza  katika  hafla hiyo   viongozi wa ngazi mbalimbali  akiwemo   Shekh Mkuu  wa  Mkoa   Shabani  bin Jumaa  na  Askofu  Mkuu  wa  Kanisa  la  Evengelisim Centre   Eliud  wamewaomba  viongozi  wa  kisiasa  na  wanaotarajia  kutafuta  nafasi za  uongozi   kuwajengea  wananchi  utamaduni  wa  kuheshimu  sheria    na  dola  iliyoko madarakani  kwani    wakizoea  kuvunja  sheria   watafanya hivyo  hata  uongozi  ulioko  madarakani ukibadilika .

Mkuu wa  mkoa  wa   Arusha  Bw  Magesa  Mulongo  amesema  upo uwezekano  wa  kuendesha  siasa, kudai  haki    na  hata  kukosoa na kutoa  mapendekezo   bila  kuvuruga amani.


Wananchi hao  wakiwa  na viongozi wa  ngazi mbalimbali  wakiwemo  wa  kisiasa ,viongozi wa dini  na  wa  mila  walikusanyika katika uwanja   huo  kuhubiri na  kuuombea  Mkoa  wa  Arusha  amani  unaoandamwa  na  heka heka za  kisiasa  ambazo zimesababisha  kuyumba kwa  uchumi.



Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger