Home » » REDDS MISS KANDA YA MASHARIKI AMBAYE PIA NI MISS MORO 2013 ASIFIWA ALIVYOJITOA KUSAIDIA WATU WENYE ULEMAVU WA VIUNGO NA MTINDIO WA UBONGO KITUO CHA AMANI.

REDDS MISS KANDA YA MASHARIKI AMBAYE PIA NI MISS MORO 2013 ASIFIWA ALIVYOJITOA KUSAIDIA WATU WENYE ULEMAVU WA VIUNGO NA MTINDIO WA UBONGO KITUO CHA AMANI.

Written By JAK on Monday, January 6, 2014 | 9:33 PM


Mrembo wa  Redds  Miss Kanda ya Mashariki , Diana Laizer , ambaye ni Miss  Morogoro 2013  akimkabidhi  zawadi ya vyakula Mkurugenzi wa Kituo cha Amani cha watu  wenye ulemavu wa viungo na mtindio wa ubongo  , Padri Beatus Sewando ( kulia) wakati alipotembelea Kituo hicho siku ya kwanza ya mwaka mpya  2014 akiwa na mshindi wa tatu wa Miss Morogoro, Muzne Abduly  pamoja na Mratibu wa  Miss Kanda ya Mashariki , Alex Nikitas ili kuwafariji na kusherekea kwa kula chakula nao.( Picha na John Nditi).
Picha ya pamoja
========  ======  =========
REDDS MISS KANDA YA MASHARIKI AMBAYE PIA NI MISS MORO 2013 ASIFIWA ALIVYOJITOA KUSAIDIA  WATU WENYE ULEMAVU WA VIUNGO NA MTINDIO WA UBONGO KITUO CHA AMANI.
Na John Nditi, Morogoro
KITUO cha Amani kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Jimbo la Morogoro  na kinachowahudumia  Watu  wenye ulemavu wa viungo na mtindio wa ubongo, kutoka sehemu mbalimbali mkoani hapa  kimepongeza  Redds Miss Kanda ya Mashariki , Diana Laizer  , kutokana na kuonesha upendo na kulijali  kundi la watu wa aina hiyo  kwa kutoa msaada wa  vyakula.
Pongezi hizo zilitolewa na Mkurugenzi wa Kituo hicho,  Padri Beatus Sewando , siku ya kwanza ya mwaka mpya 2014,  kwa Miss Kanda ya Mashariki  ambaye pia ni Miss Morogoro 2013.
Mrembo huyo ambaye  kwa sasa ni Mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) siku hiyo alikitembelea  Kituo hicho  akiwa na   mshindi wa tatu Miss Morogoro, Muzne Abduly , pamoja  na  Mratibu wa Miss Kanda ya Mashariki, Alex Nikitas ambapo alitumia siku hiyo kula na kucheza nao burdani za ngoma.
 Mkurugenzi wa Kituo hicho  alisema ,  watoto wenye ulemavu wa viungo na mtindio wa ubongo wanayo mahitaji  mengi ukiwemo kuwaonesha  upendo na wanapotembelewa  na wageni hasa nyakati za sikukuu na kupatiwa  zawadi  wanapata faraja kubwa kwa kujiona nao ni sehemu ya jamii.
“ Binafsi yangu nikiwa Mkurugenzi wa Kituo hiki , walengwa na wazazi wao tumefurahi na tumefarijika  kwa uamuzi wako kututemebela siku ya mwanzo ya kuanza mwaka huu wa 2014 , umetuletea zawadi ya vyakula” alisema na kuongeza.
  Japo wewe mwenyewe umesema ni kidogo , lakini kwetu sisi tunakiona ni kikubwa , watoto wamefurahi , kutoa ni moyo na si utajiri , kikubwa umejitoa kujakushinda nasi  leo hii” alisema Padri Sewando.
 Hata hivyo alisema , kituo hicho cha Amani kina  watoto 42  wenye ulemavu wa viungo na mtindio wa ubongo na hakina ufadhili wa n je  na wadani , kinawategemea watu wenye kujitoa na kitendo cha Miss Kanda ya Mashariki kukitembelea na kutoa zawadi ya vyakula ndiyo ufadhili wenyewe.
Pamoja na hayo alisisitiza kwa kusema “ Kituo hakina ufadhili na nina  waomba wote wanaoshinda kuwa Miss Morogoro  waige mfano wa Miss Diana , ambaye amejitoa  na kuutumia muda wake  kusaidia jamii  isiyojiweza” alisema na kusisitiza kuwa.
“ Jambo hili ni kubwa na linayapa hadhi  mashindano haya  ambayo  jamii yetu  siku zote imekuwa na  fikra potufu ya kuwa Ma Miss  ni wapenda  starehe na anasa, lakini sivyo ilivyo miaka ya hivi sasa ” alibainisha.
Naye Redds Miss Kanda ya Mashariki, alisema kuwa , moja ya majukumu yake ni kusaidia jamii hasa makundi ya watoto yatima na wenye ulemavu sambamba na wanaishi  katika mazingira magumu , wakiwemo wa Kituo hicho.
Hivyo alisema, kwa kutambua jukumu hilo, siku hiyo ya mwaka mpya aliamua kukitembelea Kituo hicho  na kutoa  msaada wa vyakula ,kula nao na kuburudia kwa pamoja ili kuonesha upendo.
Hivyo alitoa wito kwa washiriki wengine wa Urembo wajitokeza kusaidia makundi kama hayo kile kidogo wanachokuwa nacho kwani wao pia ni sehemu ya jamii inayohitaji kutunzwa kiafya , kielimu na kijamii.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger