Home » » WATANZANIA DMV WATOWA POLE KWA WAFIWA

WATANZANIA DMV WATOWA POLE KWA WAFIWA

Written By JAK on Monday, January 6, 2014 | 9:27 PM


 Rafiki wa mpendwa wetu Catherine Nyongole akishindwa kujizuia  mara tu alipomuaona mdogo wa marehemu Ngalu Buzohera alipofika nyumbani kwa marehemu kutoa pole na kujumuika nao katika kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na mpendwa wao Zainab Buzohera aliyefariki jana jioni Jan 4, 2014 katika hospitali ya Doctor's Community iliyopo Goodluck Rd, Lanham, Maryland. Msiba upo nyumbani kwa wafiwa 5030 57th Ave, Bladensburg, Maryland na leo baadae kutafanyika harambee ya kuchangisha fedha ilikusaidia kuusafirisha mwili wa marehemu harambee itafanyika 5401 Anapolis Rd, Bladensburg, Marland kuanzia saa 10 jioni(4pm) Lengo ni kujitahidi kumsafirisha mpendwa wetu siku ya Jumatano Jan 8, 2014.Watanzania wakiamua hawashindwi na jambo.
 Watanzania wa DMV wakijumuika na wafiwa nyumbani kwa marehemu.
 Catherine Nyangole mwenye kilemba cheusi pamoja na WanDMV wakimpa pole mdogo wa marehemu Ngalu Buzohera nyumbani kwa marehemu.
 Watanzania wa DMV wakiendelea kutayarisha makulaji kwa ajili ya wageni watakaofika nyumbani kuwapa pole wafiwa.
 Watanzania DMV wakijumuika pamoja na wafiwa nyumbani kwao
Watanzania wa DMV wakiwafariji wafiwa.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger