Home » » CRDB YATOA MILIONI 100 KUSAIDIA WALIOPATWA NA MAFURIKO MKOANI MOROGORO

CRDB YATOA MILIONI 100 KUSAIDIA WALIOPATWA NA MAFURIKO MKOANI MOROGORO

Written By JAK on Thursday, February 6, 2014 | 6:04 AM

Rais  Jakaya Kikwete akimkaribisha ikulu jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei, (kushoto), alipofika kutoa msaada wa sh. milioni 100 kwa ajili ya kusaidia waathirika wa mafuriko yaliyozikumba wilaya tatu za Kilosa, Mvomero na Gairo katika Mkoa wa Morogoro, mwezi uliopita. Dk. Kimei alifuatana na baadhi ya viongozi wa benki hiyo.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (kushoto), akisalimiana na Rais Jakaya Kikwete ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk. Charles Kimei.
Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa.ikulu jijini Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Bernki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kulia), Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa, wakimsikiliza Rais Jakaya Kikwete (hayupo pichani), ikulu jijini Dar es Salaam., 
Dk. Kimei akifafanua jambo kwa Rais Jakaya Kikwete.
Mazungumzo yakiendelea.
Dk. Charles Kimei akitoa maelezo mafupi kabla ya kukabidhi hundi ya Sh, milioni 100 kwa ajili ya wahanga wa mafuriko yaliyotokea mkoani Morogoro.
Rais  Jakaya Kikwete akipokea hundi ya sh. milioni 100 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kushoto), kwa ajili ya kusaidia watu waliopatwa na mafuriko Mkoani Mororo hivi karibuni. 
Rais Jakaya Kikwete akiangalia kwa makini hundi aliyokabidhiwa.
Rais Jakaya Kikwete akiiweka katika bahasha hundi ya Sh, milioni 100 baada ya kupokea kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (kushoto), huku  makini hundi aliyokabidhiwa, Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka
Rais Dk. Jakaya Kikwete akimkabidhi hundi aliyokabidhiwa na uongozi wa Benki ya CRDB kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi anayeshughulikia pia masuala ya maafa, William Lukuvi.
Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei.
Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka akiwa katika picha ya pamoja na Rais Jakaya Kikwete.
Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Njia Mbadala za Kibenki katika Benki ya CRDB,  Joseph Witts. 
Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu (kulia), akiwa  na Rais Jakaya Kikwete.
Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Katibu wa Benki ya CRDB, John Lugambo.
Rais Dk. Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Benki ya CRDB, Kushoto ni Katibu wa Benki ya CRDB, John Lugambo, Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk. Charles Kimei, Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka, Mkurugenzi wa Idara ya Njia Mbadala za Kibenki,  Joseph Witts na Meneja Uhusiano wa Benki ya CRDB, Godwin Semunyu. 
Rais  Jakaya Kikwete (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Benki ya CRDB mara baada ya kupokea hundi ya sh. milioni 100 kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei (wa pili kushoto), kwa ajili ya kusaidia watu waliopatwa na mafuriko Mkoani Mororo hivi karibuni. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvispan style="background-color: white; text-align: start;">, Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma Shirikishi wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka (wa pili kulia), na Mkurugenzi wa Masoko Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa. 
Rais Dk  Jakaya Mrisho Kikwete akimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei, baada ya kukabidhiwa hundi ya shilingi milioni 100  kutoka benki hiyo kusaidia waathirika  wa mafuriko yaliyozikumba wilaya tatu za Kilosa, Mvomero na Gairo katika Mkoa wa Morogoro
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger