Home » » RAISI JAKAYA KIKWETE AZINDUA MABANGO YA KUHAMASISHA WANANCHI KUPIGA VITA MAUAJI YA TEMBO,FARU

RAISI JAKAYA KIKWETE AZINDUA MABANGO YA KUHAMASISHA WANANCHI KUPIGA VITA MAUAJI YA TEMBO,FARU

Written By JAK on Wednesday, February 12, 2014 | 11:45 PM

 Moja ya mabango yaliyozinduliwa na Rais Jakaya Kikwete usiku wa kuamkia leo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam kwa ajili ya kuhamasisha wananchi kupiga vita mauaji ya Tembo na Faru nchini. Hafla hii ilifanyika muda mfupi kabla Rais Kikwete hajapanda ndege kuelekea London, Uingereza, kuhudhuria mkutano wa kimataifa wa kupanga mikakati ya kupambana na ujangili na biashara haramu ya meno ya tembo na faru.
 Rais Jakaya Kikwete (kulia) akibofya kwenye kompyuta kuzindua rasmi  mabango hayo ya kuhamasisha wananchi kupiga vita mauaji ya Tembo na Faru  kwenye  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Mahamoud  Mgimwa. 
 Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa uzinduzi wa mabango ya kuhamasisha wananchi kupiga vita mauaji ya Tembo na Far baada ya kuyazindua rasmi kwenye  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam 
 Moja ya mabango hayo likiwa nje ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam
 Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa uzinduzi wa mabango ya kuhamasisha wananchi kupiga vita mauaji ya Tembo na Farubaada ya kuyazindua rasmi kwenye  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam. Kulia ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Jambo Concepts Tanzania Limited, Juma Pinto. Kulia kwake ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Dk. Mahamoud  Mgimwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Said  Meck Sadick.
Share this article :

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. New EAC Blog - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger