Mkurugenzi. mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Mizinga Mwelu (kushoto), akisalimiana na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, John Mongela wakati mkurugenzi huyo alipometembelea mkuu huyo wa mkoa kwa lengo la kufahamiana, jijini Arusha.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania, Mizinga Melu
(kulia), akimsikiliza Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha na ambaye pia ni Mkuu wa
Wilaya hiyo, John Mongela wakati mkurugenzi huyo alipofika kwenye ofisi za mkuu
wa mkoa huyo kujitambulisha. Katikati ni Meneja Mkuu wa Mawasiliano wa
NBC,William Kallaghe. Bi. Mizinga pamoja na kujitambulisha lakini pia alielezea
mipango na mikakati ya NBC kwa mkuu huyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Tanzania , Mizinga Melu
(kushoto) akimwelekeza mmoja wa wateja wa benki hiyo, Hangi Donald Kiloba,
jinsi ya kupata huduma za kibenki za NBC kwa kupitia mitandao ya simu za
mkononi (NBC Mobile Banking) kwenye tawi la benki hiyo la Uhuru jijini Arusha
mwishoni mwa wiki. Wateja wa NBC wanashauriwa kuendelea kwenda katika matawi ya
benki hiyo nchini kote kuunganishwa na huduma hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC, Mizinga Melu (kulia)
akimsalimia mmoja wa wateja wa benki hiyo, Christopher Cyprian katika tawi la
NBC la Uhuru jijini Arusha. katikati ni Meneja wa tawi hilo, Aliko Mwamusaku .
Mkurugenzi aliwambia wateja tawini hapo kujiunga na huduma za kifedha za NBC
kwa kutumia mitandao ya simu za mkononi (NBC Mobile Banking) ili kupata huduma
za kibenki na pia kufanya malipo ya huduma mbalimbali kutoka kwa watoa huduma
watakaounganishwa na NBC Mobile banking.
Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Uhuru mkoa wa Arusha, Aliko
Mwamusaku (kushoto) akimtambulisha Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Mizinga
Melu (katikati) kwa mmoja wa wateja wa benki hiyo Sijohn Chembakassery wakati
wa ziara ya mkurugenzi huyo tawini hapo jijini Arusha.
Na Michuzi Blog
Post a Comment