Na.Tamimu Adam - Jeshi la Polisi.
JESHI Polisi Mkoani Mtwara
limefanikiwa kukamata gari lenye
namba za usajili T.867 aina ya Toyota Carina Saloon likiwa limebeba shehena ya mifuko yenye meno ya Tembo tisini (90) yenye uzito wa kilogramu 222.1 ya
thamani zaidi ya shilingi bilioni moja (1,082, 025,000/=)
Akizungumzia tukio hilo, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mtwara
Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Zelothe Steven alisema kuwa gari
lilikamatwa Kata ya Maendeleo, wilaya ya Masasi katika barabara kuu ya Tunduru kuelekea
Masasi.
Zelothe alisema kuwa askari wa doria walilitilia shaka gari
hilo na kumuamuru dereva kusimama
kuonyesha leseni ya udereva ambapo dereva wa gari hilo hakuwa nayo, ndipo
askari alichukua hatua yakufanya ukaguzi ambapo alikuta gari hilo limejaza shehena ya
mifuko inayosadikiwa kuwa ni meno ya Tembo.
“Askari waliamua
kulifisha gari hilo kwenye kituo kikuu cha Polisi wilaya ya Masasi umbali wa
kilometa moja kutoka sehemu lilipokamatwa gari hilo, wakati wakiwa njiani
kuelekea kituoni dereva na mwenzake walikuwa wakimshawishi askari huyo
waelewane ili wampatie shilingi milioni tatuaweze kuwaachia lakini askari huyo alikataa na kufanikiwa
kulifikisha gari hiyo kituoni” Alisema Zelothe.
Alisema kuwa kabla gari hilo halijasimama vizuri dereva na
mwenzake waliruka na kutokomea
vichochoroni, juhudi za kuwasaka bado zinaendelea ili waweze kukamatwa na kufikishwa mahakamani.
Miongoni mwa vitu vilivyokutwa ndani ya gari hilo wakati wa
upekuzi ni pamoja na simu moja ya kiganjani aina ya Techno, mizani aina ya
tonash, fomu za “notification” pamoja
na Bank slip.
Kutokana na uchunguzi uliofanyika imebainika kuwa dereva wa
gari hilo anatajwa kuwa ni Oliver Lucas
mkazi wa Masasi na mwenzake aliyekuwa naye bado hajatambulika na inaaminika kuwa tajili wao ni
mtu mwenye jina la Hassan Koko anayejulikana kwa jina
maarufu la Twalib Nyoni.
Kamanda Zelothe amewataka wananchi kuongeza kasi ya kutoa
taarifa za uhalifu na wahalifu ili kuwezakukomesha biashara hii haramu
ya usafirishaji wa nyara za
Serikali na kutoa taarifa
itakazowezesha kukamatwa kwa watuhumiwa hao ili
waweze
kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Na Michuzi Blog
Post a Comment