TCCIA YAADHIMISHA MIAKA 25 YA KUZALIWA KWAKE KWA KONGAMANO LA KIBIASHARA.
Chemba ya Wafanyabiashara, wenye Viwanda na Kilimo TCCIA
imesherehekea miaka 25 ya kuanzishwa kwake kwa kufanya kongamano kubwa
lililowaunganisha sekta binafsi na serikali.Mamia ya wafanya biashara na
taasisi za serikali wamejuimuika pamoja kujadiliana masuala mbalimbali na kero
zinazowakumba wafanya biashara.
zinazowakumba wafanya biashara.
Waziri Wa Viwanda na Biashara Mhe. Dr. Abdallah Kigoda(Mb)
akiongea na wafanyabiashara katika kongamano hilo.
Kogamano hili lilijadili Kero na mazingira ya kufanya
biashara Tanzania na namna yanavyowezesha
biashara kuwa na tija kwa mfanyabiashara na serikali kwa ujumla katika kukuza uchumi wa Taifa.
Wadau kutoka sekta mbalimbali kutoka taasisi za utafiti, chuo kikiuu cha Dar es Salaam, wafanyabiashara
na wadau wengine kutoka taasisi za sekta binafsi walishiriki kwa kutoa mada fupi za kuchokoza mjadala.
biashara kuwa na tija kwa mfanyabiashara na serikali kwa ujumla katika kukuza uchumi wa Taifa.
Wadau kutoka sekta mbalimbali kutoka taasisi za utafiti, chuo kikiuu cha Dar es Salaam, wafanyabiashara
na wadau wengine kutoka taasisi za sekta binafsi walishiriki kwa kutoa mada fupi za kuchokoza mjadala.
Baadhi ya Washiriki wakifuatilia kwa makini Mada mbali mbali
ambazo ziliwasilishwa wakati wa Mdahalo huo.
Mada zilizojadiliwa ni pamoja na;-
1. Kurejeshwa kwa ada za leseni za biashara na madhara yake
kwa wafanya biashara.
2. Madhara ya kanuni na sheria nyingi zihusuzo biashara na
athari zake katika mazingira ya ufanyaji wa biashara
3. Madhara ya mashine za ukusanyaji kodi kwa jumuhia ya
wafanyabiashara”
4. Madhara ya masamaha wa ushuru kwa baadhi ya biashara kwa
wafanyabiashara wa ndani ya nchi”
5. Madhara ya uwepo wa mizani nyingi za barabarani pamoja na
vizuizi vya polisi
6. Changamoto zinazowakabili wanawake wajasiriamali
wanaofanya biashara za mipakani iliyotolewa
7. Sera ya kulinda viwanda vya ndani na madhara yake kwa
wawekezaji wa ndani
Post a Comment