Paris, Ufaransa. Atletico Madrid imekuwa katika mafanikio
makubwa Hispania na Ulaya watapata zawadi yao ya kwanza leo kama watashinda
dhidi ya Austria Vienna jijini Madrid na kufanikiwa kufuzu kwa hatua ya 16 bora
ya Ligi ya Mabingwa.
Vumbi jingine litatimuka kwa kuwashusha vinara wa England,
Arsenal na mahasimu wake Chelsea wakionyesha kazi na miamba ya Bundesliga,
Borussia Dortmund na Schalke 04.
Chelsea v Schalke 04
Chelsea wataikaribisha Schalke siku chache baada ya kupokea
kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Newcastle, kipigo hicho kilimfanya Kocha Jose
Mourinho kudai alifanya makosa 11. “Tupo
katika nafasi nzuri ya kusonga mbele, lakini kama tutafungwa tena basi
tutajiweka kwenye hali ngumu,” alitadharisha Mourinho.
Basel v Steaua
Bucharest
Basel wanawakaribisha Bucharest wakiwa na rekodi mbaya ya
kutoka sare kwenye mchezo wa kwanza hivyo sasa wanapigana kuhakikisha wanapata
tiketi ya kucheza Europa Ligi.
Borussia Dortmund v
Arsenal Dortmund iliiharibu sherehe ya kuzaliwa Arsene Wenger alipokuwa
akitimiza miaka 64, waliposhinda 2-1 kwenye Uwanja wa Emirates. Dortmund
wanakwenda kwenye mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi katika Bundesliga
walipoichakaza Vfb Stuttgart 6-1.
Arsenal wenyewe walishinda 2-0 dhidi ya Liverpool.
Napoli v Marseille
Rafael Benitez ameiongoza Napoli kushinda mechi tatu
mfululizo za Serie A, na leo atakuwa mwenyeji wa Marseille ambao aliwafunga 2-1
kwenye mchezo uliopita. Matokeo hayo yameifanya timu hiyo ya Italia kuwa na
matumaini ya kufuzu kwa mtoano, akiwa sawa kwa pointi sita na Dortmund na
Arsenal, huku Marseille wakiwa hawana pointi yoyote.
Zenit St Petersburg v
FC Porto Zenit wataiacha zaidi Porto katika harakati za kusaka kufuzu kama
watashinda leo na kufanya tofauti kati yao kuwa pointi nne ikiwa wamekiza mechi
mbili. Zenit walifanya kazi ya ziada kuwafunga Porto kwenye mchezo uliopita
walikutana hivyo kuifanya mechi ya leo kuwa na utamu wa aina yake.
Atletico Madrid v
Austria Vienna Atletico imetumia vizuri udhaifu wa kundi na kujiweka katika
nafasi nzuri ya kucheza 16 bora kwa mara ya kwanza tangu msimu wa 2008/09. Pia
ushindi wa Atletico utawafanya waweke rekodi ya kushinda mechi nne mfululizo za
michuano hiyo mikubwa ya Ulaya, wakivunja rekodi yao ya kushinda mechi tatu
msimu wa1958/59.
Ajax v Celtic Ajax
inahitaji japo pointi moja ili kujiweka katika matumaini hata ya kupata nafasi
ya tatu ya kucheza Europa Ligi. Celtic wenyewe watakuwa wakisaka ushindi
mwingine dhidi ya Wadachi hao ili kufufua matumaini ya kucheza hatua ya mtoano
kwa mara ya pili mfululizo.
Barcelona v AC Milan
Barcelona bado haijawa katika kiwango chake cha juu, lakini inayo nafasi ya
kucheza hatua ya 16 bora wakati watakapowavaa wachovu AC Milan wanaondamwa
majeruhi.
Shaka ya Barcelona ni ndogo kulianganisha na Milan ambao
wameanza msimu wa Serie A vibaya zaidi baada ya miaka 20 kupitia. Kama Milan
watafungwa na Barcelona na Celtic watashinda basi nafasi yao ya kusonga mbele
itakuwa finyu zaidi.
Post a Comment