Kwa ufupi
Akizungumza wakati wa
hafla ya kutangaza ujio wa kombe hilo, Meneja Mkazi wa Coca-Cola Tanzania inayodhamini ziara hiyo, Yebeltal
Getachew alisema, Novemba 30 maelfu ya
mashabiki wa soka watapata fursa ya kulishuhudia kombe hilo katika tukio
litakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Dar es Salaam. Kombe halisi la Dunia la Shirikisho la Soka
la Dunia(FIFA)litawasili nchini Novemba 29 mwaka huu ikiwa ni sehemu ya ziara
yake katika nchi 88 duniani kote.
Akizungumza wakati wa hafla ya kutangaza ujio wa kombe hilo,
Meneja Mkazi wa Coca-Cola Tanzania
inayodhamini ziara hiyo, Yebeltal Getachew
alisema, Novemba 30 maelfu ya mashabiki wa soka watapata fursa ya
kulishuhudia kombe hilo katika tukio litakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar
es Salaam.
Getachew alisema,mgeni rasmi wakati wa ziara ya kombe hilo
hapa nchini atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete.
“Wito wangu kwa mashabiki wa soka hususani wa Dar es Salaam
wajitokeze kwa wingi wakati wa ujio wa kombe hilo hasa kutambua kwamba hii ni
fursa adimu,”alisema Getachew na kuongeza:
“Mashabiki watapata fursa ya kupiga picha, kutazama video
zinazoonyesha matukio mbalimbali ya kihistoria ya Kombe la Dunia la FIFA na
kufurahia burudani za kusisimua.”
Alisema, ujio wa kombe hilo kwa mwaka huu 2013, umezingatia
mafanikio ya ziara zingine za Kombe Halisi la FIFA zilizowahi kufanyika mwaka
2006 na 2009.
Naye Mkurugenzi wa Idara ya
Michezo, Leonard Thadeo alisema, ziara hiyo itasaidia kuitangaza
Tanzania katika medani ya kimataifa.
“Mkumbuke kwamba ujio wa Kombe la Dunia hapa nchini
utaambata na vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa hivyo ni wazi sisi kama
nchi tutapata nafasi ya kujitangaza kimataifa,”alisema Thadeo.
Post a Comment