Na Fidelis Butahe, Mwananchi
Kwa ufupi
Wakati Feleshi
akieleza hayo, Kamanda wa polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova
alisema uchunguzi wa suala hilo bado unaendelea, huku akisisitiza kuwa
atalitolea ufafanuzi leo kama akipata kibali cha kufanya hivyo na Waziri wa
Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki.
Dar es Salaam. Siku moja baada ya raia wa China kukamatwa na
vipande 706 vya meno ya tembo, Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP)
Eliezer Feleshi amesema wanasubiri uchunguzi wa suala hilo kukamilika.
Wakati Feleshi akieleza hayo, Kamanda wa polisi Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema uchunguzi wa suala hilo bado
unaendelea, huku akisisitiza kuwa atalitolea ufafanuzi leo kama akipata kibali
cha kufanya hivyo na Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki.
“Unajua ile ni ‘task force’ iliyoanzishwa na waziri
mwenyewe, na amelizungumzia, sasa mimi siwezi kusema kilichokwishazungumzwa na
waziri,” alisema Kamanda Kova. Juzi Kagasheki aliongoza operesheni ya kuwasaka
watu wanaojihusisha na ujangili katika Mtaa wa Kifaru, Mikocheni, wilayani
Kinondoni sambamba na polisi na maofisa usalama na kufanikiwa kuwakamata raia
watatu wa China, Xu Fujie, Chen Jinzha na Huang Qin wakiwa na meno hayo.
Akizungumza na gazeti hili jana, Feleshi alisema kazi yake
ni kupambana na uhalifu na kufafanua kuwa uchunguzi ukikamilika, taratibu za
kufikishwa mahakamani zitafanyika.
“Tunasubiri uchunguzi ukamilike kwanza, kisha taratibu
zingne zitafuta kwa mujibu wa sheria,” alisema Feleshi.
Meno hiyo 706 ni sawa na tembo 353 waliouawa katika hifadhi
za wanyama pori mbalimbali hapa nchini.
Post a Comment