Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Jaji Barnabas Samata (kushoto) akimtunuku Shahada ya Udaktari wa Falsafa ya Chuo Kikuu hicho, Mbunge wa Viti Maalum Pindi Chana katika Mahafali yaliyofanyika Chuoni hapo mjini Morogoro leo.
Mbunge wa Viti Maalum, Pindi Chana akishukuru baada ya kutunukiwa Shahada ya Udaktari wa Falsafa ya Chuo Kikuu cha Mzumbe na Mkuu wa Chuo hicho, Jaji Barnabas Samatta (wapili kulia) katika mahafali ya Chuo hicho yaliyofanyika chuoni hapo mjini Morogoro leo. Wa nne kulia ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda na wasita kulia ni mkewe Mama Tunu Pinda akifuatiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe Joel Bendera.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mkewe Mama Tunu Pinda wakopozi kwa furaha na Binti yao Janet Pinda ambaye alipokea Shahada ya Uzamili ya Uongozi katika Mifumo ya Afya kwenye Mahafali ya Chuo Kikuu cha Mzumbe yaliyofanyika Chuoni hapo mjini Morogoro leo.
Mtoto wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Janet Pinda (kulia) akipongezwa na wadogozake, Nasirika Nyema (wapili kulia) na Namsi Pinda (kushoto) baada ya kutunukiwa Shahada ya Uzamili ya Uongozi katika Mifumo ya Afya kwenye Mahafali ya Chuo Kikuu cha Mzumbe mjini Morogoro leo.
Mtoto wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Janet Pinda, akipongezwa na shangazi yake , Beatha Pinda Kaitira (kushoto) baada ya kutunukiwa shahada ya uzamili ya uongozi katika mifumo ya afya kwenye mahafali ya chuo kikuu cha mzumbe mjini Morogoro December
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mzee Kingunge Ngombale Mwiru katika mahafali ya Chuo Kikuu cha Mzumbe mjiniMorogoro Desemba 6, 2013. Katikati ni mkewe Mama Tunu Pinda. Picha na PMO
Post a Comment