Latest Post
7:50 AM
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI IBADA YA MAZISHI
Written By JAK on Wednesday, October 30, 2013 | 7:50 AM
YA
ASKOFU MSTAAFU, MHASHAM RAYMOND MWANYIKA ILIYOFANYIKA MKOANI NJOMBE .

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal, Spika Anne Makinda na viongozi wengine wakitoa heshima
za mwisho na kuaga mwili wa marehemu

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya Askofu
Mstaafu, Mhasham Raymond Mwanyika, wakati wa shughuli za maziko zilizofanyika
leo katika Kanisa Katoliki Njombe.

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal, Spika Anne Makinda na viongozi wengine wakielekea
kanisani kuaga mwili wa marehemu

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal, akiweka mchanga kaburini

Makamu wa Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.
Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana
na Katibu Kiongozi Mstaafu Mhe Philemon Luhanjo baada ya mazishi hayo. Picha na OMR
na Katibu Kiongozi Mstaafu Mhe Philemon Luhanjo baada ya mazishi hayo. Picha na OMR
Labels:
Africa
7:42 AM
MHE. MEMBE AKUTANA NA MKUU WA CHOMBO KIPYA CHA EU KUHUSU USALAMA MAJINI
Balozi wa Jumuiya ya Ulaya hapa nchini, Mhe. Filiberto Cerian Sebregondi (kulia) akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao kuhusu masuala mbalimbali ya Usalama Majini.
|
Mhe. Membe akimsikiliza Bw. Poncins akielezea utendaji kazi wa Chombo hicho cha EUCAP Nestor.
|
Mazungumzo yakiendelea |
Mhe. Sebregondi akichangia jambo wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Bw. Poncins (hawapo pichani)
|
Maafisa kazini! Kutoka kushoto ni Bi. Zulekha Fundi na Bw. Frank Mhina, Maafisa Mambo ya Nje wakinukuu mazungumzo kati ya Mhe. Membe na Bw. Poncins (hawapo pichani).
|
Mhe. Membe akisisitiza jambo kwa Mhe. Sebregondi na Bw. Poncins baada ya kumaliza mazungumzo yao
|
Picha ya pamoja. |
Labels:
Africa
7:35 AM
WANAHABARI IRINGA WALIBANA GAZETI LA RAI
WATAKA LITAJE MAJINA YA WAANDISHI WALIOHONGWA NA VIONGOZI WA CCM MKOA WA IRINGA
Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari mkoa wa Iringa Frank Leonard kulia akitoa msimamo wa wanahabari dhidi ya gazeti la Rai na mbunge Msigwa leo ,kushoto ni katibu mtendaji wa IPC Francis Godwin
Wanahabari Clement Sanga kushoto akiwa na mwakilishi wa New habari {2006} Ltd wachapishaji wa magazeti ya Mtanzania , Rai na Bingwa mkoa wa Iringa Mercy Mwalusamba wakati wa kikao cha cha wanahabari mkoa wa Iringa leo kujadili habari zilizoandikwa na gazeti la rai jumapili
Na Francis Godwin Blog
WANAHABARI mkoani Iringa wamekanusha vikali habari zilizoandika na gazeti la Rai toleo namba 1067 la jumapili wiki iliyopita kuwa wanahabari mjini Iringa wamehongwa fedha na viongozi wa CCM mkoa wa Iringa ili wasiandike habari ya msaidizi wa mbunge Wiliam Lukuvi Bw Thom Malenga kukamatwa kwa tuhuma za kujihusisha na ujangili.
Wahanabari hao katika kikao chao kilichofanyika leo katika ofisi za klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Iringa (IPC) mbali ya kukanusha habari hizo kuwa zimeandikwa kwa lengo la kuchafua tasnia ya habari mkoa wa Iringa ila bado wanalitaka gazeti la Rai na mbunge wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa kuwataja waandishi waliohongwa na viongozi wa CCM mkoa wa Iringa kabla ya wanahabari hao hawajachukua hatua zaidi dhidi ya gazeti la rai pamoja na mbunge Msigwa.
"Kilichoandikwa na gazeti la Rai jumapili kuhusu wanahabari Iringa hawajatutendea haki na wametuvunjia heshima yetu kwa wadau wa habari mkoa wa Iringa na nje ya mkoa wa Iringa.....ila tunachotaka Rai kuwataja waandishi hao waliohongwa ili sisi kwa sisi kama wanahabari kuanza kuchukuliana hatua ....wakishindwa kufanya hivyo ndani ya siku 14 kuanzia leo jumanne tutawafikisha baraza la habari Tanzania (MCT)"
Walisema wanahabari hao katika tamko lao la pamoja lililotolewa na mwenyekiti wa IPC Frank Leonard kuwa taarifa hiyo imechafua vibaya wanahabari Iringa na sio wacache ni wote kutokana na jinsi ambavyo gazeti hilo lilivyoandika habari hiyo tena mbaya zaidi mwandishi wa habari hiyo hakuweza kuwatendea haki wanahabari Iringa hata kwa kuonyesha kuwahoji katika habari yake hiyo.
Leonard alisema kuwa si kweli kama wanahabari Iringa walishindwa kuandika habari hiyo ya kukamatwa kwa Malenga isipo kuwa wanahabari Iringa ni makini na hawakutaka kuandika habari kwa kukurupuka hivyo walitaka kabla ya kuandika kuweza kumpata msemaji wa kikosi hicho cha kupambana na ujangili ili kulizungumzia hilo kabla ya kuandika jambo ambalo wao kama wanahabari walikuwa wakilisikia mitaani bila kuwa na uhakika.
Uandishi wa habari mzuri ni pamoja na kuzingatia maadili ya uandishi na sio kuandika bila ya kuwa na uhakika wa kile unachokiandika .
Hata hivyo alisema kwa kuwa mbunge Msigwa amenukuliwa katika gazeti hilo kama ndio msemaji wa jambo hilo wao kama wanahabari watamwandikia barua mbunge huyo ili kusaidia kuwataja wanahabari waliohongwa pesa vinginevyo wao kama wanahabari wa mkoa wa Iringa hawatamvumilia mbunge Msigwa katika hilo .
Pia alisema kuwa suala hilo kwa sasa ameachiwa mwanasheria wa IPC ili kulifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kuwaandikia barua Rai na mbunge Msigwa kuwataka kuthibitisha ukweli wa kilichoandikwa dhidi ya wanahabari mkoa wa Iringa.
Labels:
Africa
7:31 AM
Na Mwandishi Wetu, Blantyre Malawi.
MCHEZAJI wa timu ya Safari Pool Taifa, Patrick Nyangusi ameibuka Bingwa wa Afrika katika mashindano ya mchezaji mmoja mmoja(singles) wanaume yaliyojumuisha timu saba kutoka katika Nchi sita za Afrika.
Patrick Nyangusi aliupata ubingwa huo kwa kumfunga mchezaji bora wa Afrika Kusini, Vishen Jagdev 6-4,katika mchezo ambao ulisisimua wapenzi na mashabiki wengi wa mchezo huo uliofanyika katika ukumbi wa kisasa wa Roben Complex jijini Blantyre.
Nyangusi kwa ubingwa huo alizawadiwa medali ya dhahabu ambapo mshindi wa pili alichukua mpinzani wake, Vishen Jagdev kutoka Afrika Kusini ambaye alizawadiwa Medali ya Silver wakati mshindi wa tatu ni Moses Mofya kutoka Zambia ambaye alimfunga mchezaji wa Tanzania, Omary Akida, 5-3 na hivyo Moses Mofya kuzawadiwa Medali ya Fedha na nafasi ya nne ilichukuliwa na mchezaji kutoka Tanzania, Omary Akida.
Upande wa timu zilizowakilisha Nchi, Zambia waliibuka mabingwa katika mchezo ambao uliendeshwa kwa mfumo wa ligi ambapo Zambia waliongoza kwa pointi 14.
Nafasi ya pili ilichukuliwa na timu kutoka Nchi ya Afrika Kusini kwa pointi 12,na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Nchi ya Tanzania ambao walipata pointi 9, wakati nafasi ya nne ilibaki kwa wenyeji Malawi ambao walipata pointi 4.
Akizungumza Mkurugenzi wa mashindano ya AAPA (All Africa Pool Associations), Rick Schoenlank, alizipongeza Nchi zote zilizoshiriki mashindano hayo,pili aliwapongeza waandaaji wa mashindano kwa maandalizi mazuri na mwisho aliipongeza Tanzania kwa kutoa bingwa wa Singles kwamwaka 2013.
Nae mgeni rasmi aliyefunga mashinndano hayo, Mjumbe wa Baraza la Michezo la Nchini Malawi, Sharaf Pinto, kwa niaba ya Waziri wa michezo wa Malawi,aliipongeza pia Tanzania kwa kutoa bingwa Singles na kuwaomba Tanzania kuwa karibu na wachezaji wa Malawi ili kubadilishana uzoefu na udugu pia kwa kutembeleana na kucheza mechi za kirafiki.
Lakini pia aliwapongeza Zambia kwa kutwaa ubingwa wa timu na vilevile aliwapongeza Malawi kwa nafasi waliyopata si mbaya sana, ni nafasi ambayo inawafanya wajiandae vyema kwa mashindano yajayo.
Mwisho aliwapongeza kila Nchi kwa kuleta uwakilishi na kuwatakia safari njema ya kurejea Nchini salama mpaka mashindano mengine mwakani.
Mashindano ya mwaka huu yalijumuisha Nchi takribani 6, ambazo ni Afrika Kusini, Zambia,Tanzania,Lesotho,Namibia na wenyeji Malawi 1 na Malawi 2.
Timu ya Safari Pool ililiyokwenda Malawi ina jumla ya wachezaji 8, ambao ni Mohamed Idd, Patrick Nyangusi Festo Yohana ,Mereczedec Amadeus,Omary Akida,Abdalah Hussen ,Godfrey Swain a Nahodha Charles Vernas na viongozi watatu ambao ni Meneja wa timu Nabil Hiza,Katibu wa chama cha pool Taifa, Amos Kafwinga na Makamu Mwenyekiti, Fred Mush
Mashindano ya AAPA mwakani yanatarajiwa kufanyika Tanzania jijini
Dar es Saalaam.
TIMU YA TAIFA YA MCHEZO WA POOL YAFANYA VIZURI NCHINI MALAWI
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Safari Pool ya Tanzania wakiwa
na medali zao za Fedha mara baada ya kutunukiwa kwa kupata nafasi ya tatu
katika mashindano ya Pool Afrika yaliyofanyika jijini Blantyre Malawi mwishoni
mwa wiki.

Wachezaji na mashabiki wa timu ya Safari Pool kutoka
Tanzania wakishandilia na mchezaji Patrick Nyangusi mara baada ya kutwaa
ubingwa wa mchezaji mmoja mmoja (Singles) Afrika uliofanyika Blantyre Malawi
mwishoni mwa wiki.

Wachezaji na mashabiki wa timu ya Taifa ya Safari Pool ya
nchini Tanzania wakiwa wamembeba mchezaji,Patrick Nyangusi mara baada ya kutwaa
ubingwa wa Afrika wa mchezaji mmoja mmoja (Singles) kwa kumfunga Vishen Jagdev
wa Afrika Kusini 6-4,katika mchezo uliofanyika Blantyre Malawi mwishoni mwa
wiki.

Bingwa wa Afrika wa mchezo wa Pool kutoka Tanzania, Patrick
Nyangusi akicheza dhidi ya mpinzani wake, Vishen Jagdev kutoka Afrika Kusini
(hayupo pichani) wakati wa mchezo wa fainali uliofanyika Blantyre Malawi
mwishoni mwa wiki.
Mgeni rasmi,Mjumbe wa Baraza la Michezo Nchini Malawi, Sharaf Pinto(wa pili kushoto) akiwa na mabingwa wa Singles(mchezaji mmoja mmoja).Kutoka kulia ni mshindi wa tatu kutoka Zambia, Moses Mofya,mshindi wa pili kutoka Afrika Kusini, Vishen Jagdev na Bingwa gwa Afrika kutoka Tanzania, Patrick Nyangusi wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwakabidhi medali zao Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki.
Mabingwa wa Afrika wa mchezo wa pool wakiwa katika picha nya pamoja.Kutoka kushoto ni Bingwa wa Afrika kutoka Tnzania, Patrick Nyangusi,mshindi wa pili kutoka Afrika Kusini, Vishen Jagdev na mshindi wa tatu kutoka Zambia, Moses Mofya mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao jijini Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki.
Wachezaji
wa timu ya Taifa ya Safari Pool ya Tanzania wakiwa na medali zao za
Fedha mara baada ya kutunukiwa kwa kupata nafasi ya tatu katika
mashindano ya Pool Afrika yaliyofanyika jijini Blantyre Malawi mwishoni
mwa wiki.
Bingwa wa Afrika wa Safari Pool kutoka Tanzania, Patrick Nyangusi akiwa katika picha ya pamoja na warembo wa Blantyre Malawi mara baada ya kukabidhiwa zawadi ya medali ya zahabu mwishoni mwa wiki.
Na Mwandishi Wetu, Blantyre Malawi.
MCHEZAJI wa timu ya Safari Pool Taifa, Patrick Nyangusi ameibuka Bingwa wa Afrika katika mashindano ya mchezaji mmoja mmoja(singles) wanaume yaliyojumuisha timu saba kutoka katika Nchi sita za Afrika.
Patrick Nyangusi aliupata ubingwa huo kwa kumfunga mchezaji bora wa Afrika Kusini, Vishen Jagdev 6-4,katika mchezo ambao ulisisimua wapenzi na mashabiki wengi wa mchezo huo uliofanyika katika ukumbi wa kisasa wa Roben Complex jijini Blantyre.
Nyangusi kwa ubingwa huo alizawadiwa medali ya dhahabu ambapo mshindi wa pili alichukua mpinzani wake, Vishen Jagdev kutoka Afrika Kusini ambaye alizawadiwa Medali ya Silver wakati mshindi wa tatu ni Moses Mofya kutoka Zambia ambaye alimfunga mchezaji wa Tanzania, Omary Akida, 5-3 na hivyo Moses Mofya kuzawadiwa Medali ya Fedha na nafasi ya nne ilichukuliwa na mchezaji kutoka Tanzania, Omary Akida.
Upande wa timu zilizowakilisha Nchi, Zambia waliibuka mabingwa katika mchezo ambao uliendeshwa kwa mfumo wa ligi ambapo Zambia waliongoza kwa pointi 14.
Nafasi ya pili ilichukuliwa na timu kutoka Nchi ya Afrika Kusini kwa pointi 12,na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Nchi ya Tanzania ambao walipata pointi 9, wakati nafasi ya nne ilibaki kwa wenyeji Malawi ambao walipata pointi 4.
Akizungumza Mkurugenzi wa mashindano ya AAPA (All Africa Pool Associations), Rick Schoenlank, alizipongeza Nchi zote zilizoshiriki mashindano hayo,pili aliwapongeza waandaaji wa mashindano kwa maandalizi mazuri na mwisho aliipongeza Tanzania kwa kutoa bingwa wa Singles kwamwaka 2013.
Nae mgeni rasmi aliyefunga mashinndano hayo, Mjumbe wa Baraza la Michezo la Nchini Malawi, Sharaf Pinto, kwa niaba ya Waziri wa michezo wa Malawi,aliipongeza pia Tanzania kwa kutoa bingwa Singles na kuwaomba Tanzania kuwa karibu na wachezaji wa Malawi ili kubadilishana uzoefu na udugu pia kwa kutembeleana na kucheza mechi za kirafiki.
Lakini pia aliwapongeza Zambia kwa kutwaa ubingwa wa timu na vilevile aliwapongeza Malawi kwa nafasi waliyopata si mbaya sana, ni nafasi ambayo inawafanya wajiandae vyema kwa mashindano yajayo.
Mwisho aliwapongeza kila Nchi kwa kuleta uwakilishi na kuwatakia safari njema ya kurejea Nchini salama mpaka mashindano mengine mwakani.
Mashindano ya mwaka huu yalijumuisha Nchi takribani 6, ambazo ni Afrika Kusini, Zambia,Tanzania,Lesotho,Namibia na wenyeji Malawi 1 na Malawi 2.
Timu ya Safari Pool ililiyokwenda Malawi ina jumla ya wachezaji 8, ambao ni Mohamed Idd, Patrick Nyangusi Festo Yohana ,Mereczedec Amadeus,Omary Akida,Abdalah Hussen ,Godfrey Swain a Nahodha Charles Vernas na viongozi watatu ambao ni Meneja wa timu Nabil Hiza,Katibu wa chama cha pool Taifa, Amos Kafwinga na Makamu Mwenyekiti, Fred Mush
Mashindano ya AAPA mwakani yanatarajiwa kufanyika Tanzania jijini
Dar es Saalaam.
Mtaa Kwa Mtaa Blog
Labels:
Sport
7:21 AM
“If there is anything wrong with conflict, it is how we respond to them” remarked Ambassador Mulamula in her keynote address at the University of Salisbury in Northern Maryland at a panel discussion on Conflict Resolution and Organizational management on Friday October 25, 2013.
AMBASSADOR MULAMULA SHARES HER EXPERIENCE AT THE GREATLAKES WITH SULISBURY UNIVESITY STUDENTS AND FACULTY

“If there is anything wrong with conflict, it is how we respond to them” remarked Ambassador Mulamula in her keynote address at the University of Salisbury in Northern Maryland at a panel discussion on Conflict Resolution and Organizational management on Friday October 25, 2013.
Addressing students and faculty, Ambassador Mulamula shared
her experience as the first
Executive Secretary of the International Conference on the
Great Lakes Region (ICGLR) from 2006 to 2011, stating that unlike the learned
Salisbury community, she doesn’t study conflicts, she “live
them”
She explained the meaning of her name “Mulamula” an
arbitrator, a plant that is planted on the ground after mediation of land dispute is concluded. She added even with
such a name, she still faces, like many others, challenges that exist in managing
the humanistic instinctively reaction to conflicts.
“We often respond to conflicts instinctively, therefore we miss
the opportunity to harness the goods that may come out of a conflict” she said.
Linking her message with recent global changes which she
explains make it more difficult for organization Executives to manage conflicts
in their institutions and work places. She summed her speech outlining success in
mediation and facilitation as well as challenges, in a ten action points that
she believes to be helpful in managing conflicts.
Ambassador Mulamula was invited to give a keynote speech at
the Salisbury University by Jacques Koko, Assistant Professor and Director of
the Graduate Program of Conflict Analysis and Dispute Resolution at the Fulton School
of Liberal Arts at Salisbury.
After her speech, a group of panelists from the University
and the community provided some light on causes and implications of
organizational conflict, and how such conflicts can be addressed
constructively.

Labels:
Europe
7:14 AM
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI PROF. SOSPETER MUHONGO AZINDUA RASMI MRADI WA UMEME WA SUMBAWANGA - NAMANYERE

Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo katikati akishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya kulia kwake, Mbunge wa Nkasi Kusini Ally Kessy kushoto kwake na wazee wawili kulia na kushoto wakiwawakilisha wananchi wa Namanyere (Wilaya ya Nkasi) katika uzinduzi rami wa mradi wa umeme kutoka Sumbawanga hadi Namanyere Wilayani Nkasi leo tarehe 28, Oktoba 2013. Mradi huo uliogharamiwa na Serikali ya Tanzania na kukamilika hivi karibuni una gharama ya Tsh. Bilioni 4.3 na umepitia jumla ya vijiji kumi na mbili vya njiani kabla ya kutua katika Mji huo wa Namanyere uliopo Wialayani Nkasi Mkoani Rukwa. Tangu Tanzania ipate Uhuru mwaka 1961 na tangu kuundwa kwa Mkoa wa Rukwa mwaka 1974 Wilaya hiyo haikuwa na umeme jambo ambalo limepokelewa kwa shangwe na wananchi wa Wilaya hiyo.

Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo na washirika wake katika uzinduzi huo wakibofya kitufe maalum kama ishara ya kuwasha umeme katika Mji wa Namanyere leo tarehe 28, Oktoba 2013 baada ya Wilaya hiyo kukosa huduma hiyo katika kipindi chote cha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania. Katika uzinduzi huo Prof. Muhongo amesema Mkoa wa Rukwa umetengewa zaidi ya Tsh. bilioni 30 kwa ajili ya umeme vijijini kupitia REA, Wakala wa Umeme Vijijini ambapo jumla ya vijiji 66 katika kipindi cha miezi 20 ijayo kuanzia Novemba mwaka huu 2013 vitanufaika na mradi huo.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akimkaribisha Katibu Tawala Mkoa huo Alhaj Salum Mohammed Chima kuwasalimia wananchi wa Kirando katika ziara ya kikazi ya siku mbili ya Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo Mkoani Rukwa. Katika ziara yake hiyo anatembelea miradi mbalimbali ya umeme pamoja na kuzungumza na wananchi.

Meneja Mahusiano wa Shirika la Umeme nchini TANESCO Bi. Badra Masoud akisherehesha baadhi ya mambo katika hafla fupi ya uzinduzi wa mradi huo uliofanyika Namanyere Wilayani Nkasi leo tarehe 28, Oktoba 2013.

Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiongea na baadhi ya viongozi wa Serikali ya Mkoa wa Rukwa na Wilaya ya Nkasi leo tarehe 28, Oktoba 2013 juu ya upatikanaji wa umeme katika bandari mpya inayoendelea kujengwa ya Kipili Wilayani humo. Alisema kupitia REA, Wakala wa umeme vijijini kuanzia mwezi Desemba miradi mbalimbali itaanza kufanya kazi kuweza kufikisha umeme katika maeneo tofauti Mkoani Rukwa ikiwemo bandari hiyo ya Kipili.

Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo akiwa ameshikilia kinyago cha mfano wa mtoto na mmoja ya wanakikundi cha ngoma za asili cha Kanondo cha Mkoani Rukwa baada ya kufurahishwa na uchezaji wa ngoma ya kikundi hicho inayoelezea malezi bora kwa watoto.

Waziri Muhongo katika mikutano yake na wananchi hakusita kuwainua Mameneja wa Tanesco kuelezea juu ya miradi mbalimbali ya umeme Mkoani Rukwa. Kulia ni Meneja wa Tanesco Kanda ya Nyanda za Juu Magharibi Bi. Salome Nkondola na katikati ni Meneja wa Tanesco Mikoa ya Rukwa na Katavi.

Picha ya pamoja kati ya Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo na baadhi ya viongozi wa chama na Serikali wa Mkoa wa Rukwa.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)
Labels:
Africa